Ndivyo Baba yangu wa Mbinguni atakavyowatenda ninyi,msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake, (Mathayo 18;35).
Ni maombi yangu kwa Mungu aunyooshe moyo wangu,wanaponikosea wengine nisiishie kusamehe na nikabaki na machungu
akaseme na wewe pia kupitia ujumbe huu AMEN.
Producer - Mixing Doctor
Director - Avie
Lyrics
Nimewasamehe,Nimewasamehe
Ila tatizo kuachilia,Mungu nifundishe kuachilia.
Nimewasamehe,Nimewasamehe
Ila tatizo kuachilia,Mungu nifundishe kuachilia.
Hivi ni nani daktari wa ugonjwa wa moyo nimjue,
Anitibu tafadhali huu mzigo mzito niutue.
Maana maumivu ni makali nahitaji ukweli niongee,
Kusamehe mi sijali ila kuachilia ndo nashindwa.
Baba naona giza kwenye msamaha wangu ,na msamaha wako wewe haupo hivyo,Ukisamehe unafuta na kusahau.
Hivyo najidunduliza kijae kibubu changu , cha msamaha japo kifike hata robo,Nikisamehe nifute na kusahau.
Maana kiukweli nimesamehe ila nikikumbuka mojo unadunda TiTiTi,Nataka nisahau ili nikikumbuka hali iwe shwari.
Nimewasamehe,Nimewasamehe
Ila tatizo kuachilia,Mungu nifundishe kuachilia.
Baba wapo wale niliowakopesha wakanidhurumu
Tena wapo wale hawakujua kosa wakanihukumu
Baba wapo wale niliowapenda wakanisaliti
Tena wapo wale niliowapa siri wakazisambaza eeh
Haya ni maombi yangu Baba yangu eeeh
Nikisamehe ponya maumivu kwenye moyo wangu,
Hata nikiwaona nisije kukumbuka mabaya yao.
Pia ni maombi yangu Baba yangu eeh
Pia wanisamehe kwa yote mabaya nilotenda,
Hata wakiniona wasije kukumbuka mabaya yangu eeeh.
Baba naona giza kwenye msamaha wangu ,na msamaha wako wewe haupo hivyo,Ukisamehe unafuta na kusahau.
Hivyo najidunduliza kijae kibubu changu , cha msamaha japo kifike hata robo,Nikisamehe nifute na kusahau.
Maana kiukweli nimesamehe ila nikikumbuka mojo unadunda TiTiTi,Nataka nisahau ili nikikumbuka hali iwe shwari.
Nimewasamehe,Nimewasamehe
Ila tatizo kuachilia,Mungu nifundishe kuachilia.
Nimewasamehe,Nimewasamehe
Ila tatizo kuachilia,Mungu nifundishe kuachilia.